AUNT EZEKEL ATOA YA MOYONI TENA,SAFARI AWAGUSA NA WASANII WA BONGO MOVIE

Msanii wa Filamu Bongo, Aunt Ezekiel ameeleza sababu za baadhi ya wasanii wengi wa Bongo Movie kukimbilia katika matukio ya kisiasa.
Muigizaji huyo amesema kukosa kazi kunapelekea hilo kwa asilimia kubwa pamoja na umaarufu ambao una sababisha msanii akifanya kidogo tu inaonekana amejitoa sana upande huo. “Ni kutokana na kukosa kazi kwa sababu mwisho wa siku kazi zetu zimekuwa hazina ushindani, tumesimama katika kazi zetu, so tunajikuta hata yale ambayo hayatuhusu tunaenda kuyaingilia” Aunt Ezekiel ameiambia Times Fm.
Ameendelea na kuongeza kuwa, ‘na kwanini unaona ni Bongo Movie ndio wanashiriki, siyo kwamba ni wao tu, unaweza kukuta wananchi wengi wanashiriki lakini sisi ni puplic figure ukishiriki hata kidogo inaoneka umeshiriki kikubwa”. Hata hivyo amesema kwa upande wake kwa sasa amejitenga mbali kidogo na mambo ya siasa kwa vyama vyote na hajafanya hivyo tangu kumalizika kwa Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015.
>

No comments: