Mwigizaji Ray Aanika Siri Ya Maisha Yake, Ipo Hapa

Mwigizaji wa filamu za kibongo Vicent Kigosi maarufu kama Ray amefichua siri ya maisha yake na kubainisha kuwa alikua mtukutu enzi alipokuwa mtoto.

Akipiga stori na moja ya chombo cha habari hapa nchini Ray ameyataja baadhi ya mambo aliyokuwa akiyafanya alipokuwa shule ikiwemo kukaa nyuma kabisa ya darasa kwa wale wanafunzi wanaojulikana maarufu kwa kupiga kelele, (backbencher) na kuwa wa kwanza kutoka nje kabla ya muda muafaka kufika.

Amesema alipohitimu elimu ya sekondari alifeli na kupaa division four, lakini kitendo hiko hakikumkatisha tamaa na kufeli maisha.

Ray kwa sasa ni mwigizaji maarufu wa filamu mwenye kampuni ya utengenezaji filamu inayoitwa RJ akiwa na msanii mwenzake maarufu kama Johari.

Ray amefanya filamu kadhaa toka enzi ya Steven Kanumba alipokuwa hai ambapo kwa sasa Ray afanya vizuri na filamu ya gatekeeper. 
Download App Yetu  >> BOFYA HAPA << Tukutumie Habari na Burudani Zote FASTA Kila Time BURE Kabisa ! >

No comments: