Waziri Jafo: Taarifa Za Watumishi 2058 Walioajiriwa Wizara ya Afya Zimekamilika

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Mhe. Selemani S. Jafo (Mb) amesema jumla ya watumishi wa Sekta ya Afya wapatao 2058 wamekwisha pangiwa vituo vya kazi kuanzia leo 06/11/2017 na taarifa zote zinapatikana kwenye mtandao wa Ofisi ya Rais TAMISEMI.

“Taarifa ya watumishi 2058 imekamilika na itarushwa kwenye mtandao wa OR TAMISEMI leo tarehe 6/11/2017 jioni, hivyo Makatibu Tawala wa Mikoa na Wakurugenzi wa Halmashauri zote nchini wanatakiwa kujiandaa kuwapokea watumishi hao ikiwemo kuwapatia stahiki zao”

Amewataka Wakurugenzi wa Mamlaka za Serikali za Mitaa na Waajiri kuhakikisha wanachukua taarifa za watumishi walioripoti na kuwaingiza kwenye Mfumo wa Mishahara na kuwapangia katika maeneo ambayo ya uhitaji mkubwa ili kuboresha huduma za afya nchini.

Pia ameekeza watumishi wanaopangiwa vituo, kuripoti katika vituo vyao vya kazi ndani ya siku 14 tangu tangazo hili kutolewa.

Aidha, Waajiri wote watoe taarifa juu ya kuripoti kwa watumishio haa wapya na vituo walivyopangiwa siku 14 baada ya kuripoti kwao.

Taarifa za Watumishi hao na Vituo vyao vya kazi, inapatikana katika Mtandao wa Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR TAMISEMI) wa www.tamisemi.go.tz
>

No comments: