Patrick Kanumba Kurudi Tena Kwenye Soko la Filamu

Patrick Kanumba Kurudi Tena Kwenye Soko la Filamu
Msanii wa filamu, Othman Njaidi a.k.a Patrick Kanumba ambaye ni zao la marehemu Steven Kanumba amefunguka ujio wake katika tasnia hiyo.

Patrick amesema mwakani anatarajia kurejea katika filamu baada ya kujikita katika masomo kwa kipindi kirefu na kazi tayari zimeshafanyika.

“Mpaka sasa nipo kimya ila soon inshallah Mungu akifanya wepesi tunaanza mwakani rasmi upya, nilikuwa nasoma na bado mimi ni wanafunzi,” Patrick ameiambia Bongo5.

Katika hatua nyingine amesema kuna uwezekano wa kuja kufanya tena kazi na Jennifer ambaye waliigiza wote movie ya Uncle JJ na marehemu Kanumba.

“Zipo nyingi sana kama tulivyokuwa shule kazi nyingi zinakuwa zinajitokeza sema kwa sababu tuliamua tujikite kwanza kwenye masomo, kwa hiyo kazi nyingine tukawa tunaziacha na tunashuru Mungu waliokuwa wanataka kutupa kazi walikuwa wanatuelewa” amesisitiza Patrick. 
>

No comments: